Tuesday, July 26, 2016

NIAMINI lyrics by Professor Jay

[Hook – Professor Jay] x2
Niamini (sema)
Nataka uwe na mimi (mama)
Watu wenye fitina wanaleta majungu uachane na mimi (ye ye ye)
Hivi kwanini (sema)
Hutaki kuniamini (mama)
Nyoyo ziko pamoja mpaka siku ya kifo uanze we au mimi (ye ye ye)

[Verse 1 – Professor Jay]
Nakupenda sana ingiwa wanakuita demu wa uswazini
Penzi lako la kweli ndo kitu nachothamini
Kipepeo cha moyo we sema unachotaka
Jinsi unavyoenzi kipenzi sina mashaka
Tulipanda milima tukaja kwenye mabonde
Na sasa ni tambarare tufanye wanga wakonde
Kote tunakopita wamemwagia mbigiri
Njoo nikumbatie tufe tukiwa wawili
Hushangai, tukigombana tu wanafurahi
Na tukiwa pamoja wanashindwa kutusabahi
Walishakuja kwangu kunipa habari zako
Nikawatoa mbio kulinda heshima yako
Kwangu wamenishindwa wamegeuza kibao
Changanua mapema upime akili zao
Ni maisha yo Liz, twende tujikongoje
Maisha safari ndefu sijui mbele kukoje
Wanasema mi nakunywa wee, nalala kwenye baa
Wanasema mi ni bingwa la ngono kwenye mitaa
Wanasema mi nimeshawataka wamekataa
Kwako napiga goti yoh twende ki-superstar

[Hook – Professor Jay] x2
Niamini (sema)
Nataka uwe na mimi (mama)
Watu wenye fitina wanaleta majungu uachane na mimi (ye ye ye)
Hivi kwanini (sema)
Hutaki kuniamini (mama)
Nyoyo ziko pamoja mpaka siku ya kifo uanze we au mimi (ye ye ye)

[Verse 2]
Yoh, nikwamba
Mi nashukuru sana, umeniamini kwa sana
Hukufata maneno ya wanga waliochonga kwa sana
Miss Manana baab kubwa, hiyo ndo dhana
Wala hukunikana asante sana mi sitokukana
Tulifarakana tulikaa chini, tukapatana
Bila kugombana na ndio maana hatujatengana
Tukasamehana bila kutosana, endelea kukazana
Visa vizabina maji ya shingo sa chupi zinabana
Vichwa vinagongana wanaulizana, hatujaachana
Wanapigwa na bumbuwazi kuona bado tunakumbatiana
Tunashirikiana, na tunafanya vitu vya maana
Na haki ya Mungu mi nakuahidi mi ndo wa dhamana
Nakata mzizi wa fitina we ni wangu wa kuzikana
Mwingine hakuna, vita vya manyoya sasa hapana
Kwani maneno yalizidi hasa kwa wanga na mahasidi
Na wengine waliahidi lazma watumwagie acid
Eti hakomi kutupwa na napiga sana mchupa
Hautachukua round kwangu mi ntakutupa
Haukufanya pupa haukuogopa, haukunitupa
Ya Mungu mengi leo hii mambo ni super
Na yote aliyoahidi kwangu mi lazima kukupa
Usiwe na pupa, tulia, mi ndo simba
Unanipaga hamu, na hilo napenda ufahamu
Nakumbuka maneno yako matamu, mi nakupenda wewe
Unanipa kiwewe, ubavu wangu wa pili ni wewe
Napenda uelewa, niamini ni mimi na wewe

[Hook – Professor Jay] x2
Niamini (sema)
Nataka uwe na mimi (mama)
Watu wenye fitina wanaleta majungu uachane na mimi (ye ye ye)
Hivi kwanini (sema)
Hutaki kuniamini (mama)
Nyoyo ziko pamoja mpaka siku ya kifo uanze we au mimi (ye ye ye)

[Verse 3]
Amini amini, tuko pamoja safarini
Wala sigeuki, nipo pamoja na wenye chuki
Hivi ujabaini? Wanakudanganya maneno lukuki
Eti napenda chini, eti nakuhasi na hugutuki
Hivi inaingia akilini? Ni muda gani na ni lini!
Siku hiyo hatukuwa pamoja? Kama si huzushi ni nini?
Wanga wanajikongoja navyokupenda kwa ukalando
Mwana wametunga hoja, tutengane iwe furaha
Iwe tazamia vioja, usiwaamini hata mara moja
Wengi ni vizabi zabina, wapiga majungu na wafitina
Magwiji washirikina, pima vyema tena kwa kina
Tusije tukaachana, tutawapa msemo wageni iwe meno
Itakuwa haina maana, mara tu tumefarakana
Pia itakuwa aibu, tujaribu tu kuvumiliana
Mapenzi ni taratibu, mambo ya jana sio ya leo
Tusije tukaharibu, hebu sikia sogea karibu
Nani wa kunigiribu? Kwako sioni, sisikii
Ukiacha utaniadhibu, we nipe raha, nipe zabibu
Mpaka ntakapokufa, tushirikiane kuziba ufa
Wanga wasitufate, nafurahi unavyonipenda
Sinyo nasema asange, we nipe denda, nipe mate
Mama subiri fungate, mzizi wa fitina tena tukate
Wewe na mimi (mimi), niko radhi kula yamini
Wewe na mimi (mimi), mama Lily hebu niamini

No comments:

Post a Comment