Thursday, July 21, 2016

NILIZAMIA lyrics by Lady Jaydee ft Machozi

Kumbe nilizama kwa brother meni
Kumbe nilizama kwa sista duu
Kumbe nilizama kwa brother meni
Kumbe nilizama kwa sista duu

Sijui niseme nini moyo wangu unyamaze
Au sifa zako hadharani nizieleze
Sema unachotaka utapata wangu mpenzi
Siku zote nimekuweka moyoni
Lakini bado wewe waniumiza
Kwanini mimi wanifanyia hivyo?
Wenye mimi kila siku nalia
Kwa sababu yako oh wewe
Oh mamii

Ushamba gani huo lakini!
Kosa ni kukupenda au nini?
Unaonyesha message zangu kweli! Inahusu nini?
Kuniweka speaker phone (inamaanisha nini?)
Nilidhani wa kutoka shamba tu ndo washamba
Kumbe hata mjini he-he-heiya (loh!)
Matusi kila kukicha, kubembeleza kusokwisha
Tafuta wa kuchoresha, Jay Dee nimechoka

Kumbe nilizama kwa brother meni
Kumbe nilizama kwa sista duu
Kumbe nilizama kwa brother meni
Kumbe nilizama kwa sista duu

Brother meni anadai kuwa eti ananipenda mimi
Huku nyuma ya mgongo wangu anatoka na jirani
Anawatuma washikaji zake kwangu
Anatafuta kisa ili anibwage
Anawatuma washikaji zake kwangu
Anatafuta kisa ili anibwage

Eh eh nyumbani kwetu maa nilikutambulisha
Na marafiki zangu walikupenda sana
Lakini moyo wangu umeuumiza
Mapenzi ya kisista duu sitaki tena
Mama wee, Samu mimi naumia

Nashindwa kusema, nikisema labda sitaeleweka
Mapenzi jamani yamejaa visa ndugu yangu
Oh unaemupenda huenda asikupende
Usiemupenda akuganda, ganda, ganda kama gundi
Kukuacha nimeshindwa, kuendelea pia visa kibao
Mmh naumia

Kumbe nilizama kwa brother meni
Kumbe nilizama kwa sista duu
Kumbe nilizama kwa brother meni
Kumbe nilizama kwa sista duu

Yelelele tunakuja eh, tunakuja kivingine eh
Machozi Band twakuja yeh, tunakuja kivyetu vyetu
Yele maa tunakuja eh, tunakuja kivingine eh
Machozi Band tunakuja yeh, tunakuja kivyetu vyetu
Na Nure tena (mama)
Anakuja (mama)
Machozi Band (mama)
Inakuja (mama)
Ale Lady Jay Dee, Jay Dee (mama)
Anakuja (mama)
Toto Gardner (baba)
Anakuja (baba)

Kusema unaweza utanipa mapenzi
Ni mapenzi gani ya kibrother meni yoyo
Umechemsha, na haina kwere

Machozi Band (mama)
Inakuja (mama)
Ale Lady Jay Dee, Jay Dee (mama)
Anakuja (mama)
Toto Gardner (baba)
Anakuja (baba)

No comments:

Post a Comment